MKURUGENZI MTENDAJI MHA. RAMADHANI MTINDASI AKIKAGUA ZOEZI LA ULAZAJI WA BOMBA
04-07-2026 21:10:53
Mkurugenzi Mtendaji Mha. Ramadhani Mtindasi akikagua Zoezi la ulazaji wa bomba kubwa la HDPE lenye kipenyo cha inchi 8" linaloungwa katika Kisima kilicho chimbwa mwaka 2025 Mei ambacho kilikuwa hakijaendelezwa kilichpo eneo la Mwankoko kinachotarajiwa kuongeza uzalishaji wa maji kwa lita 133,000, kukamilika kwa kazi hii kutaongeza asilimia za upatikanaji wa maji kwa Manispaa ya Singida kutoka 40 ya sasa na kufikia 50, hii itapelekea kuimarisha hali ya upatikana wa maji na kupunguza nakisi kati ya uzalishaji na upatikanaji wa maji, kazi hii inategemewa kukamilika mwezi huu Julai 2026, maeneo yatakayo nufaika na kupunguza migawo ya maji ni pamoja na Zone A linalohudumiwa na tenki la Mandewa na kusambaza huduma maeneo ya Unyankhae, Unyinga, Mizani, Njuki, Mtipa, Sabasaba,Unyakumi, Mwaja, Mandewa Rufaa,Mamise, Utemini, Jovena, Maasai,Manga na Bomani.